www.kiredioblog.blogspot.com
Kenya huenda ikajiondoa kwenye mashindano ya Olimpiki
yaliyoratibiwa kufanyika Brazil endapo hakutakuwa na suluhu dhabiti ya kuzuia
kuenea kwa virusi vya Zika.
Mwenyekiti wa kamati ya olimpiki ya Kenya bwana Kipchoge
Keino amenukuliwa akisema kuwa taifa hilo bingwa wa dunia katika riadha huenda
likajiondoa ilikuzuia kuhatarisha maisha ya wanariadha wake wasiambukizwe
maradhi ya homa ya Zika ambayo imeenea nchini Brazil.
- Ugonjwa huo wa Zika ambao huambukizwa na mbu husababisha madhara mabaya kwa watoto ambao huzaliwa wakiwa na ubongo mdogo zaidi ya kawaida.
''Hatuwezi kuwapeleka wanariadha wetu Brazil iwapo mlipuko
wa ugonjwa wa Zika hautadhibitiwa'' alisema Kipchoge Keino
- Juma lililopita shirika la Afya Duniani WHO lilitangaza hali ya tahadharikwa umma kufuatia kuenea kwa virusi vya Zika hadi Marekani na mabara mengine.
Vilevile ugonjwa huo ulizua taharuki baada ya kupatikana
kwenye manii mate na hata kwa jasho ya mtu aliyeambukizwa.
Hakuna dawa yeyote ya kutibu ugonjwa huu kwa sasa wala
hakuna kinga ila kuzuia usiumwe na mbu.
- Brazil imekuwa ikisisitiza kuwa ugonjwa huo hautaathiri wanariadha na mashabiki watakaohudhuria mashindano hayo ya olimpiki yaliyoratibiwa kuanza mwezi Agosti mwaka huu.
Kamati ya kimataifa ya Olimpiki IOC, imesema kuwa inaendelea
kushauriana na kamati andalizi ya Rio2016 kwa nia ya kutathmini tishio la
kuenea kwa ugonjwa huo.
Brazil imesema kuwa maeneo yatakayotumika katika mashindano
hayo ya Olimpiki yatakuwa yakichunguzwa kila siku hadi wakati wa mashindano
hayo.
Kenya ndio bingwa mtetezi wa riadha duniani na iwapo
itajiondoa kutoka kwenye mashindano hayo basi athari yake itakuwa wazikatika
riadha.
No comments:
Post a Comment