December 28, 2016

MAMBO SITA YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHAGUZI ENEO LA BUSTANI


 MAMBO SITA YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHAGUZI ENEO LA BUSTANI

Kwa mafanikio ya kilimo cha bustani ni muhimu sana kuzingatia uchaguzi wa eneo, hii itapelekea zao Fulani kutoa mazao mazuri kutokana na uchaguzi mzuri wa eneo, kwa kuzingatia sifa zifuatazo za eneo hilo.
Chagua eneo lenye sifa zifuatazo.

1.HALI YA HEWA.
Hali ya hewa hapa vipengele vifuatavyo vinahusishwa joto (Temperature), mvua (rainfall) kiasi cha unyevu katika anga (humidity), kasi ya upepo (wind), zote hizi ni vitu vya kuzingatia sana katika uchaguzi wa eneo, mazao mengi yana mahitaji tofauti ya hali ya hewa hivyo kukufanya ewe mkulima kuwa mwangalifu katika hill.
2.AINA YA ZAO
Aina ya zao pia ni kitu kingine cha muhimu sana, mazao na eneo hupelekea mafaniio ya kilimo sio mazao yote yanaleta fauda kubwa hivyo chagua zao ambalo litaendana na faida kwa kushirikisha na uchaguzi wa eneo pamoja na soko lako.

3.CHANZO CHA MAJI.
Maji ni uhai wa bustani na maji hayo yawe na sifa zifuatazo yawe yanapatikana kwa kipindi chote cha msimu wa uzalishaji, maji yawe yenye ubora na sio yaliyo changanyika na kemikali, ambazo huenda yakaleta madhara kwa matumizi ya binadamu.

4.UPATIKANAJI WA VIBARUA.
Wafanyakazi kwaajili ya kufanya shughuli mbalimbali za shamba ikiwemo palizi, upuliziaji wa dawa shamba na hata uvunaji.

5.URAHISI KUFIKA SOKONI.
Ufikaji wa mazao sokoni ni jambo pia la kuzingatia, kuanzia usafirishaji.

6.AINA YA UDONGO.
Kila zao lina aina yake ya udongo kwaajili uzalishaji utakaoleta mazao mazuri, hivyo zingatia sana aina ya udongo, kuna aina kuu tatu za udongo mfinyanzi, kichanga, na tifutifu,
Udongo wa mfinyanzi hufaa sana mazao kama kitunguu, mpunga kwani udongo huu hutuamisha sana maji, udongo wa kichanga hufaa kwa mazao kama karroti, udongo wa tifutifu huu ni udongo ambao mazao mengi hustawi sana kwani ndio udongo unaoshauriwa sana kitaalamu kwa mavuno bora.

No comments:

Post a Comment

Harmonize Ft Diamond Platnumz Kwangwaru